KUOA SIOI TENA!



                                                                                  
Janajike hili limeniparamia na kuniporomosha kihela pasi huruma yoyote. Nimekuwa shangingi wake kwa muda hata kumwacha nahisi kana kwamba nautema ulimwengu ulionilea. Ubabe wake umekuwa chanzo cha majonzi yangu huke matarajio yangu ya kimaisha nayo yamekuwa giza totoro. Demu huyu ni   ni jangili wa kimabavu kutokana na hila zake za kinyama. Vyombo vyangu vimekuwa vyake, nguo zangu nazo zimekuwa zake na si hayo tu, maisha yangu ameyamiliki hadi salamu nipatazo kutoka kwa akina dada wengine huwa chanzo cha kukurupushwa naye. Nimekuwa mtumwa nyie ndugu zangu!
Kwanza aingiapo chumbani mwangu salamu nizipatazo huacha akili yangu iki-hang. Marashi ambayo huwa ameyamimina kwa makwapa yake kwa wakati mwingine hunifanya nizirai. Kumbuka hata hayo marashi yalikuwa yangu hapo awali kwani niliyaiba kwa babangu kutokana na ile hali ya kuwa hawezi nipa mapeni nikanunue. Baada ya salamu yake kama kawaida huanza kunung’unika namna njaa invyombwaga, ‘haki baby njaa inaniua, si twende Sowe.’ Moyoni kwa wakati huo najiambia ‘huyu mpumbavu hajui sina pesa.’kudhihirisha ujinga wangu kwa maswala ya mapenzi nitampongeza kwa hilo swala lake onevu. Baadaye hulia mvunguni mwa kitanda kwani ile shilingi mia moja ambayo ingenipa gorogoro moja ya mahindi ya kusiaga ilikuwa imeshanyakuliwa na hili jinamizi.  Tuendapo huko kununua chips huwa amenishika kwa mikono yake miwili kiunoni akiwaonyesha watu hii ni mali yangu binafsi na hamjakaribisha.
Jamani nimenyonywa damu na pia kimfuko. Mwili wangu umekuwa wa kijeneza karibu nafa. Janajike hili limekuwa funza kwangu wa kuninyonya kimawazo pia. Anapopagawa hujipachika viguo vifunikavyo sehemu core ilhali sehemu elective huziacha. Vitambaa hivi hunitia kiwewe  kwani huwa vina maringo kwa sehemu nyingine za mwili kwani huzibagua tu. Nimekuwa mtumwa wa kuuficha uchi wake kila mara. Dada huyo amen’roga mie mashangingi! Ni baradhuli lisilo na bunduku bali bugdha za mama Mabruki wa Burundi. Pahala popote lipitapo lawaroga hilo Janajike langu. Si mavazi, si umbo, si marashi, yote yajiuza kivyao bila kujitembeza. Mapenzi yake yameoza na pia ni ya kidumba ambayo huwa ni ya kunitia kiwewe. Amenisakama kwa namna zote hali ambayo imenilemaza na kunifunga minyororo mazito kama ya nanga.   
Jamani kwa wale ambao wanataka kujitosa katika haya mazoeano ya mapenzi bandia nawashauri mpitie kwangu huku Kibera yaani jumba la H lango la mwisho kabisa niwashauri ya kuzingatia. Ikiwa watarajia tafadhalia lazima uwe tayari kwa yafuatayo; kutumia hela zako kumshibisha hata ikiwa wahisi njaa, kumpigia simu kiholela hata ikilazimisha  kukopa okoa jahazi, kutokula mboga nyakati hizo za mapenzi hafifu.  Si hayo tu, kuulizwa maswala balagha kila wakati, ‘uko wapi na uko na nani hapo,’ na pia swala la kugombezwa wakati wowote ule hasaa ikiwa umekata mawasiliano naye. Mapenzi ya hapa chuoni ni kama mchezo wa kalongolongo ambao huweza anza wakati wowote halafu baadaye kwa muda mfupi tu walemazwa kwa vishindo. Kawaida yanapoanza mabusu nashangwe za kikike huwa ndizo tarumbeta ya kitambulisho yake ilhali yapogonga mwamba watu huchaniana nguo. Hapo ndipo watagundua ya kuwa walikuwa wajinga. Utamsikia mmoja wao akisema, ‘kumbe sikujua kama yule Moshe ni mjinga kiasi kile.’
Kwa kweli mapenzi huweza kuwa kidonda na usipojihadhari utakuwa kidonda wewe mwenyewe. Kwangu naona uhuni kwaniweza. Nanyi dada zangu kwaherini tutaonana ahera wakati wa kichapo.

Comments

Popular posts from this blog

Does degree worth it?

Kisa cha Suleiman bwana Hamisi-kwa wapenzi wa Kiswahili pekee.