SIASA CHAFU



                                                                   
 Hizi ndizo nyakati ambazo cheche za maneno zilizouchi na zisotimilifu zitamwagwa hapa na pale kwa watu wenye kiu kama mimi na wewe. Humu nchini usishangae kuwaona vigogo wa kisiasa wakijikusanya kwa misingi ya kikabila pasi kuzingatia misingi-endeleo ya nchi. Wanasiasa ni watu ambao wanamaradhi ya sintofahamu bin sahau na hata baada ya machafuko yal’oshuhudiwa miaka ya 2007/2008 hawakushtushwa hata ncha. Mwanasiasa ni pandikizi la mtu ambaye huwa mwingi kwa wakati fulani ilhali baadaye huadimika. Anapokuwa kwa ombaomba zake huonekana kama ambaye anashida nyingi zinazomnyonga na kumsomba kiakili. Nyakati hizo huonekana mwehu kwani ahadi wanazotupa huweza kumchanganya hata Mola mwenyewe. Wanaweza kukuahidi ahera japo wao ni familia ya jahanamuni. Kawaida hawa ni viumbe wal’otumwa na shetani kuutwaa ulimwengu kupitia porojo zao zilizojaa fitina na ufidhuli mwingi sana. Siasa ni kama biashara au uzinifu kwani sheria zake ni za nipe nikupe yaani nipe karatasi yako ya kura nami nikuhutubie ulaghai wangu.
Kimwili huwa ni watu wenye miraba minne. Vitambi hivi huashiria ule unafiki wa hali ya juu kwani watu wa eneo bunge lao huwa wamechotwa kwa mikiki ya njaa na maradhi tetemesha. Uchi wa mwanasiasa ni hadhara kwa yeyote na licha ya hayo bado sisi hujipata tumewachagua tena. Hili huashiria namna wao hutumia dumba kwa kutusomba kimawaza. Kwa wakati mmoja mganga mmoja alikiri kuwa wateja wake wakuu ni wanasiasa haswaa wa hapa nchini Kenya. Jambo hili laonyesha namna walivyowasherati hawa wadhalimu. Kwa kawaida utawapata wakiokoka katika mikutano ya injili ovyo ovyo. Hata Mungu naye amekuwa adinasi wa kuchezewa na hawa wahalifu. Mikutano au hata janga lolote linapotokea huwa hawaachwi nyuma. Binadamu wengine sio watu. Ukiwa na kitu watakuja na unapokosa watakukimbia. Unapokuwa na kura watakukujia na unapokosa kura hiyo huku ukiwa unateseka watakukimbia hawa wanasiasa. Huu si uungwana hata kidogo!
Huwa twawaona mashujaa hao wanasiasa ilhali hatuelewi ulimwengu wao. Haya huwa ni mapenzi bandia ambayo baadaye hutuelekeza futi sita udongoni. Ulimwengu wao ni majabali ya miamba ya vyuma ambao chini umesitiriwa na vigae vya vioo ambao bilashaka waashiria pengo la kutokuwa kamilifu. Jasho la riziki yetu limekuwa dimbwi lao la kujistarehesha. Matendo yao huashiria ule ukungu wa hewa yao chafu ulivyotanda himaya ya nchi yetu. Hata mimea wameikosea kwa namna wanavyopitisha miswada inayoathiri misitu yetu iliyoshwari.
Kwa wale ambao wanania ya kujitosa katika ulingo wa kisiasa humu chuoni nawaomba mjichunguze kimienendo halafu jifokee ukiwa waona hujiwezi. Ukiwa umeoza jipeleke makavazi kwani huo ndio ulimwengu wako. Nanyi wapiga kura wenzangu pia tuwachunguze hawa adinasi ambao hutaka utajiri kwa uongo kwa kuangalia kwa umakini ukucha wao hadi unnywele ule wa mwisho. Hawa watu ni tisho kwa maisha yetu na wasipochunguzwa kwa umakini nasi tutaoza kama wao kwani samaki mmoja akioza………..! wataja tuambukiza ngoma yao kwani hata huruma hawana. Wamekuwa kama panya wanaokuuma kasha wanakupuliza. MAJINAMIZI!

Comments

Popular posts from this blog

Does degree worth it?

Kisa cha Suleiman bwana Hamisi-kwa wapenzi wa Kiswahili pekee.